
Warembo wengine waliofanikiwa kufikia fainali wanatoka katika nchi za Angola,Ethiopia,Ghana,Kenya,Mozambique,Nigeria,South Africa,Zambia na Zimbabwe.
Lilian Mduda ambaye ni mwanfunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam akisomea Biashara(B.Comm), amesema amejiandaa vyema kwa ajili ya shindano hilo na haoni mshiriki yeyote anayemtisha isipokuwa ni yeye mwenyewe anayeweza kujiwekea mazingira ya kushinda kwa kuzingatia yale yote atakayoelekezwa na kuyafanya kwa ufanisi ili aweze kufikia malengo yake katika fainali hizo.
Lilian anapenda kusoma novels zenye hadithi za kimapenzi na chakula akipendacho ni wali na maharage.Ndoto zake ni pamoja na kuweza kutembelea jiji la Paris siku moja.Pia anapenda mpira wa kikapu(basketball) na hupenda kusikiliza mziki na kujisomea.Kila la kheri Lilian.
Ukitaka kujua zaidi kuhusu Mnet Face of Africa na warembo wengine wanaoshiriki,bonyeza hapa
No comments:
Post a Comment
toa maoni yako kadri uwezavyo.