Pata habari mbalimbali za Kitaifa,Kimataifa,Michezo na Burudani Kupitia blog yako ya ukweli na uhakika BORN IN DAR

Jiwe kali wiki hii! C pwaa-Mmhh! (HD)

Thursday, January 21, 2010

SOUL LEGEND TEDDY PENDERGRASS IS NO MORE!!January 14, 2010
Kama wewe ni mpenzi wa muziki aina ya soul,bila shaka kabisa utakuwa unamtambua vyema mwanamuziki Teddy Pendergrass.
Habari za kusikitisha ni kwamba Teddy Pendergrass amefariki dunia hivi leo huko Philadelphia nchini Marekani.Kwa mujibu wa mtoto wake Teddy Pendergrass II, baba yake alifanyiwa colon cancer surgery miezi minane iliyopita na hakupona vizuri tangu hapo.Amefariki akiwa na umri wa miaka 59 katika hospitali ya Philadelphia’s Bryn Mawr.
Teddy ambaye nyimbo zake zilizojaa mahaba na bashashi zilitamba sana katika miaka ya 1970s na 1980s, alizaliwa March 26,1950 huko Philadelphia. Nyimbo kama vile “Turn Off The Lights”,”Close The Door” ni miongoni mwa nyimbo ambazo zilitokea kupendwa sana na mpaka hivi leo bado zinapendwa.
Teddy alitangaza rasmi kustaafu kutoka katika shughuli za muziki mwaka 2006 lakini akarudi tena jukwaani mwaka mmoja baadaye kwa ajili ya concert ya kuchangisha fedha kwa Taasisi yake ya Teddy Pendergrass Alliance inayosaidia watu walio na matatizo ya uti wa mgongo.
Kama utakumbuka Teddy Pendergrass mwenyewe alipata ajali mbaya ya gari mwaka 1982 ambapo aliumia vibaya uti wake wa mgongo kitu kilichosababisha alazwe hospitali kwa muda wa miezi sita.Baada ya hapo alirejea tena studio na kutoa albamu ya “Love Language”.
Pumzika kwa amani Teddy.Sikiliza wimbo wake “Close The Door” hapo chini.



1 comment:

  1. oya mzazi iyo imetulia m2 wang kep it up!im zero frm dsm

    ReplyDelete

toa maoni yako kadri uwezavyo.