Pata habari mbalimbali za Kitaifa,Kimataifa,Michezo na Burudani Kupitia blog yako ya ukweli na uhakika BORN IN DAR

Jiwe kali wiki hii! C pwaa-Mmhh! (HD)

Monday, January 25, 2010

MAUMIVU YA MIAKA”-WAGOSI WA KAYA January 24, 2010
Nina imani kwamba hujawasahau Wagosi wa Kaya.Naam ni wale wale vijana kutoka Tanga ambao miaka ileee waliingia kwenye anga za muziki kwa kishindo pale walipohoji “Tanga Kunani Pale”?
Tangu pale Wagosi wa Kaya wakawa wamejikita katika ile aina ya muziki wa kizazi kipya ambao mimi hupenda kuuita “conscious” kwa maana ya kwamba unalenga kwa undani kile kinachoendelea katika jamii.Ukipenda uite “muziki tambuzi”.
Baada ya kuwa kimya kwa miaka kadhaa(hata wao wanakiri katika wimbo huu kwamba walikuwa kimya kwa muda mrefu) wamerudi.Na mara hii wamerudi wakiwa na timing ya aina yake.Wanagusia uchaguzi,siasa na mambo kama hayo. Kama unavyojua,mwaka huu,watanzania watajipanga foleni ili kuchagua tena viongozi.Demokrasia.Wao wanasema ni Maumivu ya Miaka 10!
Wasikilize Wagosi wa Kaya kwa kubonyeza player hapo chini.Sikiliza kwa makini ujumbe kwani kwa maoni yangu,kidogo sauti ya beats ni ya juu kuliko za wanaoghani.

No comments:

Post a Comment

toa maoni yako kadri uwezavyo.