Pata habari mbalimbali za Kitaifa,Kimataifa,Michezo na Burudani Kupitia blog yako ya ukweli na uhakika BORN IN DAR

Jiwe kali wiki hii! C pwaa-Mmhh! (HD)

Thursday, February 11, 2010

CHID BEENZ KUMSHIRIKISHA T I D.

Yapo majina ya wasanii wa kizazi kipya ambao ukisikia wameshirikiana(collaborate)kutengeneza kazi fulani, basi unakuwa na imani kubwa kwamba kazi hiyo ina nafasi kubwa ya kuwa nzuri. Hiyo inatokana na uzoefu na pia zingatio za kazi zao zilizopita,nafasi waliyonayo katika uwanja mpana wa sanaa ya muziki na mambo kama hayo.
Hivi karibuni nilipoletewa kazi mpya na kuambiwa kwamba wasanii waliomo katika kazi hiyo ni TID(Top in Dar) na Chid Benz, nilikuwa na uhakika kwamba kazi hiyo itakuwa imesimama.TID na Chid ni miongoni mwa wasanii wa muziki wa kizazi kipya ambao binafsi nawaheshimu na sioni noma kusema kwamba nazipenda nyingi kati ya kazi zao.Habari nzuri ni kwamba hawakuniangusha katika kazi hii ya hivi karibuni inayokwenda kwa jina Huyu.
Kama zilivyo kazi nyingi za wasanii wetu siku hizi,hii pia ni hadithi ya mapenzi (bado natamani wigo wa yaliyomo(content) za kazi za wasanii upanuke zaidi na kugusa maeneo mengine yanayoizunguka jamii).Kinachoufanya wimbo huu uwe tofauti ni uwezo binafsi wa wasanii husika na hadithi yenyewe.
Kazi hii imepikwa pale Tetemesha Records(kule kule alikoibukia Hussein Machozi) chini ya George Mpanda au maarufu kama Kid Bwoy. Bonyeza player hapo chini usikilize wimbo Huyu

No comments:

Post a Comment

toa maoni yako kadri uwezavyo.