Pata habari mbalimbali za Kitaifa,Kimataifa,Michezo na Burudani Kupitia blog yako ya ukweli na uhakika BORN IN DAR

Jiwe kali wiki hii! C pwaa-Mmhh! (HD)

Thursday, February 11, 2010

BAADHI YA WASANII WANAMUZIKI WA MAREKANI WAKIFANYA REMIX YA WIMBO WA WE ARE THE WORLD WA HAYATI MICHAEL JACKSONI,baadhi ya wasanii ni kama usher raymond,celline dion...!
Miongoni mwa matukio ya ki-muziki ambayo yataendelea kukumbukwa kwa muda mrefu ni pamoja na tukio la jumla ya wanamuziki 45 kukusanyika katika studio za Jim Henson za jijini Los Angeles mwaka 1985 na kutengeneza wimbo ulioitwa We Are The World ambao ulikuwa mahsusi kwa kuchangia fedha kwa ajili ya Afrika na hususani nchi ya Ethiopia ambayo ilikuwa imekumbwa na ukame wa kutisha kuanzia mwaka 1984-1985.Ulikuwa ni umoja na upendo wa aina yake waliouonyesha wanamuziki wale sio tu kwa bara la Afrika bali kwa taasisi nzima ya ubinadamu. Wanamuziki Lionel Richie na Michael Jackson(RIP) ndio walioandika wimbo ule ambao ulifanikiwa kuchangisha jumla ya dola milioni 30 zilizokwenda kusaidia waathirika wa ukame ule.
Katika kujaribu kurudia kile walichofanya superstars wa ulimwengu wa muziki takribani miaka 25 iliyopita, hapo juzi jumla ya wasanii 100 (wengi wao kutoka Marekani) ambao wanatamba hivi sasa katika muziki ulimwenguni,walikusanyika katika studio moja chini ya Producer yule yule aliyefyatua We Are The World ya mwaka 1985,Quincy Jones ili kuutengeneza upya wimbo wa We Are The World(remake of We Are The World). Lakini safari hii sio kwa ajili ya kuchangia Afrika bali ndugu zetu wa Haiti ambao kama unavyojua wiki chache zilizopita nchi yao ilipata tetemeko la ardhi ambalo linahofiwa kwamba lilichukua maisha ya jumla ya watu 200,000.

No comments:

Post a Comment

toa maoni yako kadri uwezavyo.