Pata habari mbalimbali za Kitaifa,Kimataifa,Michezo na Burudani Kupitia blog yako ya ukweli na uhakika BORN IN DAR

Jiwe kali wiki hii! C pwaa-Mmhh! (HD)

Sunday, February 21, 2010

K’naan’s Waving Flags Is World Cup 2010 Official Song
Pamoja na ushabiki wote wa soka nchini ambao siku hizi umejikita sio tu katika timu za Yanga na Simba bali pia timu mbalimbali zinazoshiriki ligi kuu ya nchini Uingereza(English Premier League), bado wengi tunakubaliana kwamba hakuna tukio la soka ulimwenguni linaloshinda mashindano ya kugombea Kombe la Dunia la Soka( Soccer World Cup).
Ubishi na ushindani wa Arsenal, Chelsea, Manchester United, Liverpool, Newcastle nk unapofikia ukingoni,macho na masikio huelekezwa katika Kombe la Dunia. Pale ndipo penye msisimko wa aina yake.Vipaji visivyo vya kawaida huonekana pale. Ndoto hutimizwa pale na pia ndoto huyeyuka au kuota mbawa na kupaa kama vile afanyavyo mwewe baada ya kukidakua kifaranga.
Kama unavyojua,mwaka huu kipute kipo barani kwetu. Hii ni mara ya kwanza kwa bara la Afrika kupewa nafasi ya kuandaa kombe la dunia. Ni mwaka ambao una matumaini mapya kwani ukitazama kwa makini,bara la Afrika lina wasakata kabumbu mahiri sana wanaocheza katika vilabu mbalimbali ulimwenguni hususani barani Ulaya.Mimi sina timu huko Ulaya;ila Real Madrid na Arsenal wakifungwa huwa sijisikii raha! Utaniita mshabiki?
Sasa kama ilivyo kwa matukio mengi makubwa ya michezo duniani,muziki huwa haukosi.Kunakuwa na wimbo maalumu kwa ajili ya mashindano(tournament’s official song). Kombe la dunia pia.Kwa mwaka huu, wimbo Waving Flags (kwa Kiswahili rahisi naweza kusema Kupeperusha Bendera) kutoka kwa mwanamuziki Knaan .Huu ndio World Cup 2010 Official Song.
Knaan ni mzaliwa wa Somalia. Kwa sasa makazi yake ni Toronto,Canada. Ni miongoni mwa wanamuziki wenye asili ya Afrika wanaofanya vizuri sana katika anga za muziki ulimwenguni. Bonyeza hapa ili kutembelea tovuti yake na pia hapa ili kusoma zaidi kuhusu historia yake.
Haya sasa,wimbo huo.Tupeperushe bendera.Je Afrika tutatoka kimasomaso huko Kusini mwa bara letu? Imebaki miezi michache.Usikilize wimbo Waving Flags hapo chini

No comments:

Post a Comment

toa maoni yako kadri uwezavyo.