
Muda mchache uliopita majina ya sinema,waigizaji,waongoza sinema na vipengele vingine walioteuliwa kuwania tuzo hizo kwa mwaka huu yametangazwa. Kama ambavyo ilitarajiwa, sinema ya Avatar iliyoongozwa na James Cameron pamoja na sinema ya The Hurt Locker ambayo imeongozwa na Kathryn Bigelow(mke wa zamani wa James Cameron) ndio zimepata teuzi nyingi zaidi katika kuwania tuzo hizo maarufu ambazo zinafanyika kwa mara ya 82 (miaka 82). Movie hizo zimeteuliwa mara 9 au katika vipengele 9.
Shughuli za mwaka huu za tuzo hizo zinatarajiwa kufanyika tarehe 7 Mwezi Machi(takribani siku 33 zijazo).Zitaonyeshwa moja kwa moja(live) kupitia kituo cha televisheni cha ABC cha nchini Marekani.
Kwa orodha kamili ya Oscar Nominations kwa mwaka huu,bonyeza hapa. Je kuna movie,actor au actress ambaye ulitarajia angeteuliwa kuwania tuzo za mwaka huu ambaye hajatokea katika orodha?
No comments:
Post a Comment
toa maoni yako kadri uwezavyo.